Saturday, May 4, 2013

RONALDO AWAZUIA BARCA KUSHANGILIA UBINGWA LA LIGA

VINARA Barcelona watalazimika kusubiri kwa wiki nyingine kushangilia taji la La Liga baada ya Cristiano Ronaldo kufunga mabao mawili katika ushindi wa Real Madrid inayoshika nafasi ya pili wa mabao 4-3 wakitokea nyuma dhidi ya Real Valladolid jana.
Kama Real isingeshinda, ushindi wa Barca dhidi ya Real Betis Uwanja wa Nou Camp Jumapili ungewahakikishia taji la nne ndani ya miaka mitano, wakiwa kileleni kwa pointi 13 zaidi zikiwa zimebaki mechi nne zenye wastani wa pointi 12.
Valladolid, ambayo haijachukua pointi Bernabeu kwa zaidi ya muongo, ilipata bao la kuongoza dakika ya nane wakati Oscar Gonzalez alipomtungua kipa wa Real, Diego Lopez.
Rercord breaker: Cristiano Ronaldo scored twice to put him on 199 goals in Real Madrid colours
Mvunjaji rekodi: Cristiano Ronaldo amefunga mabao mawili na kufikisha mabao 199 Real Madrid
Power: Ronaldo climbs highest to power a header from a corner past the Valladolid keeper
Nguvu: Ronaldo akienda hewani kuipiga kichwa cha nguvu kumtungua kipa wa Valladolid

WAFUNGAJI BORA LA LIGA

44 Lionel Messi (Barcelona) 
33 Cristiano Ronaldo (Real Madrid
26 Radamel Falcao (Atletico Madrid) 
19 Alvaro Negredo (Sevilla) 
 Roberto Soldado (Valencia) 
16 Ruben Castro (Real Betis) 
15 Piti (Rayo Vallecano) 
Real ilisawazisha dakika ya 26 wakati Marc Valiente alipobabatiza shiti la Angel Di Maria na kujifunga, kabla ya Ronaldo kufunga bao lake la kwanza jana kwa kichwa dakika sita baadaye.
Valladolid ilifunga kupitia kwa Javi Guerra dakika ya 35 na Kaka akaisawazishia tena Real dakika nne baadaye.
Ronaldo alifunga tena dakika 20 kabla ya mchezo kumalizika akiunganishwa kwa kichwa kona, hilo likiwa nao la 33 kwa Mreno huyo katika msimu huu wa ligi.
Ouch: It wasn't all plain sailing for Ronaldo, however, as he spent his far share of time on the deck
Maumivu: Ronaldo kuna wakati aliumia jana

No comments:

Post a Comment