Tuesday, May 28, 2013

AIBU: VIDEO YA NGONO YA WANAFUNZI WA COLLAGE MOJA ILIYOPO DODOMA YAVUJA....WALIJIREKODI WENYEWE NA KUISAMBAZA


Baadhi ya wanafunzi  wa vyuo vikuu mbalimbali mjini Dodoma  wameoza kwa matukio machafu ya ngono..

Uchunguzi wetu umebaini kuwa siyo kila mwanachuo anayepata nafasi hiyo adimu ya kujiunga na elimu ya juu anafanya kile kilichokusudiwa, badala yake wanafanya kinyume kwa kujihusisha na vitendo haramu na hatarishi vya ngono.


Katika uchunguzi wa muda mrefu, mpekuzi blog imefanikiwa kunasa matukio mbalimbali machafu yaliyopitiliza ya vitendo vya ngono  ambapo picha  na video ya ngono   ya  wanafunzi  wanaosoma chuo/COLLAGE   moja  mjini Dodoma   imenaswa laivu....
Tarehe 20  mwezi huu wa tano,mpekuzi blog ilipokea simu kutoka  kwa mdau mmoja  ambaye  aliipasha  juu ya kuwepo kwa mkanda wa ngono  chuoni hapo ambao umerekodiwa  na wanafunzi wa chuo/COLLAGE  hiyo....
Hapa walikuwa wakitazama camera ambayo waliitegesha wenyewe
--------------
Baada ya tarifa hiyo, mtandao huu ulimteua mpekuzi  mmoja  ambaye alikabidhiwa majukumu ya kuujua ukweli ikiwa ni pamoja na kuipata video  hiyo kwa gharama yoyote kama ushahidi....

Mpekuzi huyo alifanya kama alivyoelekezwa.Tarehe 22 may alifanikiwa kuonana  na mnyetishaji huyo  ambaye alimpa mkanda mzima  wa tukio hilo..
Mazungumzo yao:

Mpekuzi: Vipi kamanda, pole na kitabu!
Mnyetishaji: Asante kaka, poleni na kazi
Mpekuzi: Asante sana, suala langu ni moja tu...ambalo ni kuipata hiyo video , maelezo mengine baadae.
Mnyetishaji: (anacheka): Kaka  dunia imeoza...chuo/COLLAGE  imegeuzwa kambi ya ngono.Watu wanabebana kama kuku, mbaya zaidi wanajirekodi  live mithiri ya wacheza xxxxxxx..

Mpekuzi: Kwanza ilikuwaje wakajirekodi?

Mnyetishaji: Unajua sisi wanafunzi   tuna ile hali ya kusifiana mbele ya wenzetu.Kwa hiyo siku ukitoka na demu, ni lazima masela wajue kama ulipiga kazi kweli au ulizingua...

Inavyoonesha  ni kwamba huyu jamaa alitaka kuwathibitishia washikaji zake kwamba alimtungua huyu dem, na ndo maana akamrekodi.

Mpekuzi: ( kicheko kikali) Dah! Wanafunzi mnambo sana aisee...!!Kumbe na wewe ni mdau.Ilikuwaje video hii ikasambaa? wakishajirekodi   hubaki kwa mwenyenayo au husambazwa kwa washikaji?

Mnyetishaji: Kaka  mimi siyo mdau na  ndo maana  nikawapa huu mchongo  ili msaidie  kulikemea hili.Wakishajirekodi, video hubaki kwa mwenye nayo tu.Ukitaka kuona  ni lazima uende kwa mwenyenayo.

Hii imevuja kwa sababu jamaa alijiamini na kuwapa washikaji zake wa karibu ambapo tangu siku hiyo video ilianza kusambaa kwa kasi.

Mpekuzi: Turudi kwenye point kaka...Ntaipataje  hiyo video  ili na mimi niamini???  

Mnyetishaji: Video ninayo, ila ni lazima unitoe kidogo, nimechacha  mwanao..!!

Mpekuzi: Aaah!  kaka  umeanza  uswahili  tena?  haya usijali, ntakutoa Dinner.

Mnyetishaji: Asante kaka, ila msinitaje.

Mpekuzi: Usijali kamanda, na ndo maana sijataka  hata kuuliza mengi kuhusu wewe.Kazi yangu ilikuwa ni kuupata mkanda basi.

Hatimaye mpekuzi wetu alifanikwa kuipata video hiyo  ya aibu.Ni ngumu sana kuamini kama wabongo tumefikia hatua hii  ya laana.


Kwa muda mrefu tumekuwa tukiripoti juu ya matukio machafu yanayotendwa na madenti kwa kuweka picha tu....Baadhi ya watu wamekuwa wakipinga na kudai kuwa  hizo  si za tanzania....

Awamu hii tutaishusha  video  hiyo  kama  ilivyo  ili  jamii  ijionee.Ni video ndefu ( saa nzima).Tumeivunja katika vipande 6.

 ----------------------------------------------------
Msimamo wa mtandao  huu:
----------------------------------------------------
Mpaka  sasa  hakuna  nchi  yoyote  ya Afrika mashariki  ambayo  inaunga  mpango  mchafu wa video za ngono......
Hivi karibuni, Wakenya 11 walinaswa  wakifanya  mapenzi  na  mbwa....Taarifa  zilisambaa kila  sehemu  na  nchi  hiyo  ilichukua  maamuzi magumu  ikiwa  ni  pamoja  na  kumtimua  yule  mzungu  aliyekuwa  akiwashawishi wakenya  hao  wafanye  hivyo......
Mwaka  jana  ilivuja  video  chafu  ya  Agness masongange....Jamii  ya  kitanzania  iliungana  kwa  pamoja  kulilaani  tukio  hilo
Leo wamenaswa  watu wa kawaida tena waliojirekodi wenyewe  kwa  kukusudia....Itashangaza sana  kuwatetea  watu kama  hawa.Kuwaumbua  ni  njia mojawapo  ya  kuthibitisha  usaliti wao katika maadili ya mtanzania......
Kwa sasa, jeshi la polisi lipo  katika  vita  kali  ya  kupambana  na  makahaba. Kwa  nini  tufurahie  kukamatwa  kwa  makahaba  na  tuwatete  hawa???

Thursday, May 9, 2013

MASHOGA YAFUMWA GESTI


MWANAUME aliyefahamika kwa jina la baba Salome, mkazi wa Tandika jijini Dar es Salaam, hivi karibuni alimdhalilisha mkewe (mama Salome) baada ya kufumaniwa gesti akiwa na mwanaume mwenzake ambapo madai yalisema, walikuwa katika hatua za mwisho za kuingiliana kimwili...
 
Aibu hiyo ya mwaka ambayo ilionekana pia kama kituko ilijiri Mei 3, mwaka huu ndani ya gesti moja maarufu iliyopo Devi’s Corner –Tandika, jijini Dar es Salaam. Awali ilidaiwa kuwa, mwanaume huyo na baba Salome mwenye mke na watoto wawili wanaomtegemea kwa kila kitu, walionekana wakiingia kwenye gesti moja ambayo pia ipo maeneo hayo hali iliyozua maswali kwa watu waliokuwa wakiwafahamu. 
 
“Unajua tatizo lilianzia wapi? Baba Salome na yule mwanaume mwenzake walionekana wakiingia gesti moja kisha wakatoka, wakaingia nyingine pia wakatoka, ndipo watu wanaowafahamu wakajiuliza kulikoni wawili hao kutembelea gesti siku hiyo, wakawafuatilia,” alisema mnyetishaji mmoja. 
Akaendelea: Lakini watu waliwafahamu kwa namna mbili tofauti, baba Salome ni mtulivu, mwadilifu, mwenzake watu wanasema ana ‘katabia’ ka kutaka kuwa faragha na  wanaume wenzake bila kujulikana nini anakitaka katika usiri huo. 
 Madai zaidi yakawekwa wazi kwamba, baadhi ya watu walikwenda kwenye gesti walizokwenda wawili hao na kuulizia nini walikuwa wanakitaka, ndipo siri ikawekwa wazi kwamba wanatafuta chumba cha kupumzika kwa siku hiyo lakini kwa sheria za Jiji la Dar es Salaam (kama siyo za nchi nzima), wanaume wawili hawaruhusiwi kulala chumba kimoja.
  
Chanzo kikasema: Wambeya wakawaona wakiingia kwenye gesti ya tukio, wakapewa chumba. Ndipo wakakimbia nyumbani kwa baba Salome na kumtonya mkewe, mama Salome kwamba mumewe ameingia gesti. 

Kichekesho zaidi kinaangushwa kwamba, baada ya kuambiwa mumewe amezama gesti, mama Salome ambaye ndiyo kwanza alikuwa amefika kutoka  kwenye mikopo ya Finca, alitoka mbio huku akisema anakwenda kumtoa sikio la kulia Kidawa akiamini mumewe ameingia gesti na mwanamke huyo. “Watu walimwambia mumewe hakuingia gesti na Kidawa bali mwanaume mwenzake. Kwanza mama Salome aliomba asitaniwe juu ya hilo, lakini akasisitiziwa,” alisema mtoa habari huyo. 
Akizungumza kwa jazba na waandishi wetu nje ya gesti hiyo, mama Salome alisema kwamba alipata taarifa siku nyingi mumewe ana ukaribu na mwanaume huyo ambaye mitaani watu wanasema  anajihusisha na vitendo vya ushoga. 
 
“Nilipozipata taarifa hizi sikuziamini, nilidhani ni Kidawa ndiyo kaingia gesti na mume wangu, maana Kidawa ndiye mbaya wangu,” alisema mwanamke huyo kisha akazama ndani ya gesti akiwa na polisi ambao haikujulikana walikotokea. 
Huku mumewe na mwanaume mwenzake wakiwa hawana hili wala lile kule chumbani, mlango ulisukumwa na kufunguka ambapo mwanamke huyo aliwakuta wawili hao wakiwa wameshavua baadhi ya nguo. 
Wote walishtuka kuona wameingiliwa!  “Yaani roho inauma sana, sijui ni kitu gani umekosa kwangu mpaka unakuja kwa mwanaume mwenzako jamani baba Salome,” alisema huku akilia mama Salome. 
Baada ya kugundua wamenaswa, mwanamke aliyekuwa na baba Salome aliangua kilio huku  akiomba kusamehewa kwa vile yeye ni mume wa mtu, lakini kilio chake hakikusikika kwa polisi ambapo waliwafunga pingu na kuwataka kuelekea katika kituo cha polisi. 
Wakati wakitoa maelezo kwenye kituo cha polisi, mwanaume aliyekuwa na baba Salome alijitambulisha kwa jina la  Julius Mwita, mkazi wa Devi’s Corner ana  mke na watoto wawili na aliwaomba sana waandishi wamhifadhi kwani wakwe zake wakimuona ‘itakula  kwake’. 
“Jamani nipo tayari kwa lolote naomba sana tuyamalize hapahapa, mimi ni mume wa mtu, wakwe zangu wananiheshimu na kunithamini sana,” alisema Mwita.  
Hata hivyo, pamoja na kilio hicho mwanaume huyo aliishia kuswekwa lupango na baadaye kuhamishiwa katika Kituo cha Polisi cha Chang’ombe kwa hatua zaidi.

Wednesday, May 8, 2013

ALBINO AFUKUZWA SHULE JIJINI MBEYA KWA MADAI KWAMBA NI MCHAWI




Amina Mwamkinga alisema tangu tarehe tisa alipofukuzwa bwenini na wanafunzi wenzie wakitaka aondoke shuleni hapo wakimtuhumu kuwa mchawi majira ya usiku hali iliyomlazimu kuomba hifadhi kwa mlinzi aliyemkubalia na kukesha naye hadi asubuhi  hali iliyopelekea kupigwa na baridi kali kutokana na kukosa nguo za kujisitiri kama Shuka nk.

Hapa Amina akimsimulia mkasa mzima mwandishi wa Mbeya yetu Joseph Mwaisango mara baada ya kupata maelezo yote ya Amina mwandishi wetu alimpigia simu katibu wa chama cha maalbino mkoa wa Mbeya afike ofisi ya Mbeya yetu ili wasaidiane kutatua tatizo hilo.

katibu wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya, Wiliamu Simwale alifika ofisi ya Mbeya yetu na kuanza kumsikiliza Amina.

katibu wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya, Wiliamu Simwale akiwa makini kumsikiliza Amina katika ofisi ya Mbeya yetu
=========  ========  ============
KATIKA Hali isiyokuwa ya Kawaida Uongozi wa Shule ya Sekondari Hollwood iliyoko Mlowo Wilayani Mbozi Mkoa wa Mbeya imemsimamisha shule Mwanafunzi wa kidato cha tatu kwa takribani Miezi Miwili kwa madai kuwa anajihusisha na imani za Kishirikina.
  
Mwanafunzi huyo aliyejulikana kwa jina la Amina Mwankinga(20) ambaye ni mlemavu wa ngozi(Albino) alisimamishwa shule na uongozi wa Shule hiyo tangu Machi 9, Mwaka huu baada ya uongozi wa Shule hiyo kupata taarifa kutoka kwa Wanafunzi wakimtuhumu Mwenzao huyo kuwa ni Mshirikina.
  
Uongozi wa Shule hiyo baada ya kupata taarifa hizo ulimwamuru mhanga wa tukio hilo kuondoka Shuleni hapo pasipo kufuatilia na kujua ukweli wa jambo hilo na kupata udhibiti hivyo kumwacha Mwanafunzi huyo akizurura mitaani asijue hatma ya maisha yake.
  
Mhanga wa tukio hilo Amina Mwankinga alisema tangu tarehe tisa alipofukuzwa bwenini na wanafunzi wenzie wakitaka aondoke shuleni hapo majira ya usiku hali iliyomlazimu kuomba hifadhi kwa mlinzi aliyemkubalia na kukesha naye hadi asubuhi  hali iliyopelekea kupigwa na baridi kali kutokana na kukosa nguo za kujisitiri kama Shuka nk.

Anasema kutokana na hali hiyo Walimu pamoja na uongozi wa Shule hiyo haukuchukua hatua yoyote jambo lililomlazimu kuondoka Shuleni hapo  baada ya kukosa msaada ambapo alirejea Jijini Mbeya anakoishi na Binamu yake.
  
Binti huyo anayesomeshwa na Shirika la Under the SameSun  iliyoko Jijini Dar Es Salaam aliwaambia waandishi wa habari kuhusu mkasa uliompata huku akiomba msaada kwa wasamaria wema kumtafutia Shule ili aendelee na masomo kwa ajili ya kujiandaa na mtihani wa kidato cha nne Mwakani.
  
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya HollyWood Ambukeghe Mtafya, alipopigiwa simu kuhusu tuhumahizo alikiri kulijua suala hilo na kwamba walimrudisha mwanafunzi huyo nyumbani ili kumnusuru na kipigo kutoka kwa wanafunzi wenzie na kuongeza kuwa aliambiwa atafute shule nyingine ili ahamie.
  
Naye katibu wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya, Wiliamu Simwale  alisema alikuwa  halijui suala hilo na kwamba kama lingekuwa suala liko nyeti angejulishwa yeye juu ya hatua zilizofikiwa ambapo Uongozi wa Shule umeendelea kupokea fedha za malipo ya Mwanafunzi pasipo kutoa taarifa kwenye shirika linalolipa.

Mlezi wa Wanafunzi hao kutoka Shirika la Under the Samesun Omary Mfaume amesema kwamba hana taarifa zozote  kuhusiana na tukio hilo na kuongeza kuwa anawasiliana na uongozi wa Shule moja kwa moja ili umweleze juu ya kilichotokea ili taratibu za kumtafutia Shule nyingine zifanyika haraka ili Mwanafunzi aendelee na masomo kama kawaida.

Saturday, May 4, 2013

RONALDO AWAZUIA BARCA KUSHANGILIA UBINGWA LA LIGA

VINARA Barcelona watalazimika kusubiri kwa wiki nyingine kushangilia taji la La Liga baada ya Cristiano Ronaldo kufunga mabao mawili katika ushindi wa Real Madrid inayoshika nafasi ya pili wa mabao 4-3 wakitokea nyuma dhidi ya Real Valladolid jana.
Kama Real isingeshinda, ushindi wa Barca dhidi ya Real Betis Uwanja wa Nou Camp Jumapili ungewahakikishia taji la nne ndani ya miaka mitano, wakiwa kileleni kwa pointi 13 zaidi zikiwa zimebaki mechi nne zenye wastani wa pointi 12.
Valladolid, ambayo haijachukua pointi Bernabeu kwa zaidi ya muongo, ilipata bao la kuongoza dakika ya nane wakati Oscar Gonzalez alipomtungua kipa wa Real, Diego Lopez.
Rercord breaker: Cristiano Ronaldo scored twice to put him on 199 goals in Real Madrid colours
Mvunjaji rekodi: Cristiano Ronaldo amefunga mabao mawili na kufikisha mabao 199 Real Madrid
Power: Ronaldo climbs highest to power a header from a corner past the Valladolid keeper
Nguvu: Ronaldo akienda hewani kuipiga kichwa cha nguvu kumtungua kipa wa Valladolid

WAFUNGAJI BORA LA LIGA

44 Lionel Messi (Barcelona) 
33 Cristiano Ronaldo (Real Madrid
26 Radamel Falcao (Atletico Madrid) 
19 Alvaro Negredo (Sevilla) 
 Roberto Soldado (Valencia) 
16 Ruben Castro (Real Betis) 
15 Piti (Rayo Vallecano) 
Real ilisawazisha dakika ya 26 wakati Marc Valiente alipobabatiza shiti la Angel Di Maria na kujifunga, kabla ya Ronaldo kufunga bao lake la kwanza jana kwa kichwa dakika sita baadaye.
Valladolid ilifunga kupitia kwa Javi Guerra dakika ya 35 na Kaka akaisawazishia tena Real dakika nne baadaye.
Ronaldo alifunga tena dakika 20 kabla ya mchezo kumalizika akiunganishwa kwa kichwa kona, hilo likiwa nao la 33 kwa Mreno huyo katika msimu huu wa ligi.
Ouch: It wasn't all plain sailing for Ronaldo, however, as he spent his far share of time on the deck
Maumivu: Ronaldo kuna wakati aliumia jana

KABURI LA KANUMBA LAGEUZWA KITEGA UCHUMI, SASA UKITAKA KULIONA NI LAZIMA ULIPE TSHS 5,000/= KWANZA..!


KATIKA kile kinachoonekana kwamba ni wizi mtupu, baadhi ya vijana wanaojifanya kutunza Makaburi ya Kinondoni wamebuni njia ya kuwaibiawatu kwa kutumia kaburi la nguli wa filamu za Kibongo, marehemu Steven Kanumba.Vijana hao hujipatia kipato kwa kuwatoza watu wanaofika makaburini hapo shilingi 5,000 kwa ajili ya kuliona na kupiga picha na kaburi la nguli huyo.  Utafiti uliofanywa na Risasi Jumamosi umebaini kwamba wageni wanaotoka nje ya Dar ndiyo wanaoongoza kwa kulizwa zaidi.
Sosi wetu ambaye naye alilizwa, alisema kuwa alishangazwa kwa kutozwa fedha na vijana hao lakini hakuwa na budi kufanya hivyo yeye na wenzake ili kutimiza lengo la kulitembelea kaburi hilo la kipenzi chao.
Baada ya kupata habari hizo, gazeti hili liliunda kikosi kazi cha waandishi wake na kwenda kuwanasa vijana hao.




WAANDISHI WATINGA MAKABURINI
Alhamisi iliyopita, waandishi wetu walifika katika Makaburi ya Kinondoni na kukutana na jamaa kibao waliokuwa wakijishughulisha na kazi za ujenzi wa makaburi na kupanda maua ambapo walimchagua mmoja wao aliyejitambulisha kwa jina la Mdenmark ili kuongea na wageni nao.



WAPANGA DAU

Baada ya kuwaita chemba, jamaa huyo alianza kuwapiga somo waandishi wetu na kuwaambia kwa kuwasaidia wampe shilingi 5,000 ili kuwaonesha kaburi na kuwapa historia ya marehemu tangu enzi za uhai wake mpaka alipokutwa na umauti huku akiwatahadharisha wafanye jambo hili kuwa siri.



MCHEZO WAMALIZWA

Baada ya kukubaliana kiasi hicho cha fedha, waandishi walimpatia Mdenmark kiasi cha fedha na akachukua jukumu la kuwapeleka mahali lilipo kaburi hilo. 
Wakiwa kaburini kwa Kanumba, waandishi wetu kwa kutumia ustadi mkubwa walifanikiwa kumpiga picha tapeli huyo akiwaelekeza mambo kadhaa juu ya marehemu na picha nyingine zikimuonesha akipokea fedha kutoka kwa waandishi.

TAMKO LA MHARIRI
Si sawa kulipa fedha kwa ajili ya kuliona kaburi la Kanumba, mara kadhaa waandishi wetu wamemsikia mama mzazi wa marehemu Kanumba, Flora Mtegoa akisema kuwa hafahamu mradi huo.
Ni jukumu la Jeshi la Polisi chini ya Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, DCP Suleiman Kova kuwanasa wajanja hao.

MWALIMU WA MADRASAT ALIYEMLAWITI MWANAFUNZI AFUNGWA JELA MIAKA 15 HUKO ZANZIBAR

BAADA ya mahakama ya mkoa Vuga kumwachilia huru mwalimu wa madrasat Qadiria iliyopo Amani wilaya ya Mjini Unguja, aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kumlawiti mwanafunzi wake wa kiume wa miaka 11, hatimae mahakama kuu ya Zanzibar imemfunga jela miaka 15.

 Uamuzi huo wa mahakama umekuja kufuatia rufaa iliyowasilishwa mahakamani hapo na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP),  kupinga hukumu iliyotolewa na mahakama ya Mkoa.

 Pamoja na adhabu hiyo, mahakama imemtaka kulipa fidia ya shilingi 500,000 dhidi ya mtoto huyo mdogo aliyemfanyia kitendo hicho.

 Mahakama hiyo, chini ya Jaji Abdulhakim Ameir Issa imelazimika kutoa adhabu hiyo baada ya kuridhika na sababu za rufaa zilizowasilishwa na DPP, ambazo zilidai kuwa mahakama ya mkoa Vuga imekosea kisheria katika utoaji wa hukumu.

Hivyo, baada ya kusikiliza kwa kina hoja za pande mbili hizo juu ya rufaa hiyo pamoja na kuangalia vielelezo vya ushahidi vilivyotolewa katika mahakama ya mkoa wakati wa usikilizwaji wa kesi ya msingi, Jaji Abdulhakim alisema mahakama ya mkoa ilikosea kisheria katika utoaji wa hukumu.

Jaji huyo alilazimika kutengua uamuzi wa mahakama ya Mkoa na kumtia hatiani Ustadh huyo dhidi ya shitaka hilo la kumuingilia mtoto wa kiume kinyume cha maumbile lililokuwa likimkabili.

 "Mahakama inatengua uamuzi wa mahakama ya mkoa kwa sababu ilikosea kisheria katika utoaji wake wa hukumu, hivyo mahakama hii inaamuru kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 15, haki ya rufaa ipo wazi kwa upande ambao haukuridhika na uamuzi huu," alisema Jaji Abdulhakim.

 Sambamba na adhabu hiyo, Jaji Abdulhakim alimtaka Ustadhi huyo kulipa fidia ya shilingi 500,000 kwa mtoto huyo aliyemfanyia kitendo hicho.

 Katika rufaa hiyo upande wa DPP uliongozwa na Mwanasheria wa serikali Maulid Ame Mohammed, kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka.

 Ustadh Hamadi Bakari Mohammed, miaka 48, alikuwa akikabiliwa na kesi ya kumuingilia kinyume cha maumbile mwanafunzi wake wa kiume wa miaka 11, kesi ambayo ilikua chini ya hakimu Makame Mshamba Simgeni wa mahakama ya mkoa Vuga.

 Kesi hiyo ilifunguliwa kwa mara ya kwanza Julai 7, 2011 ambapo alikana shitaka hilo baada ya kusomewa na Mwanasheria wa serikali Juma Msafiri Karibona, kutoka ofisi ya DPP.

 Pamoja na kukana huko, upande wa mashitaka uliwasilisha mashahidi sita mahakamani hapo, lakini walishindwa kuthibitisha kosa hilo kwa mujibu wa hakimu Makame Mshamba Simgeni kwa maelezo kuwa ushahidi wao ulijaa shaka ya maana.

 Hivyo, Januari 18 mwaka jana, mahakama hiyo ya mkoa ilimuona hana hatia dhidi ya kesi hiyo na kumuachilia huru chini ya kifungu cha 219 cha sheria za mwenendo wa jinai (CPA) namba 7/2004 sheria za Zanzibar.

 Wakati mahakama hiyo ya mkoa ikitoa hukumu hiyo, mshitakiwa huyo alikuwa nje kwa dhamana ya fedha taslimu shilingi 150,000 kwa wadhamini wawili pamoja bondi ya shilingi 300,000 kwa upande wake.

 Kwa upande wa mahakama kuu, Jaji Abdulhakim alimwachilia kwa dhamana ya wadhamini wawili wenye vitambulisho, mmoja kwa fedha taslimu shilingi 1,000,000 na mwengine kwa bondi ya shilingi 300,000.

 Ilifahamishwa, kinyume na kifungu cha 132 (1) sheria namba 6/2004 sheria za Zanzibar, Januari 13, 2011 majira ya saa 2:30 za asubuhi, huko Amani alimuingilia kinyume cha maumbile mtoto huyo wa kiume (jina tunamuhifadhi).

 Pamoja na adhabu hiyo aliyopewa na mahakama, Ustadh Hamad aliwahi kukaa rumande kwa muda wa siku 16, baada ya upande wa mashitaka kupinga kupatiwa dhamana kwa mara ya kwanza alipofikishwa mahakama ya mkoa, kwa madai anaweza kuingilia kati upelelezi ambao kwa wakati huo ulikuwa bado haujakamilika.

Friday, May 3, 2013

LUGE KUMJIBU LADY JAY DEE JUMATATU

Kwenye kipindi cha Power Breakfast kitakacho rushwa siku ya jumatatu saa mbili asubuhi Ruge Ataongelea issue ya Jay Dee ,Lady Jay Dee ameingia kwenye vita kali na Clouds Fm huku akimshambulia Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba kwa madai kuwa ndio wanaokula jasho la wasanii.

MAJAMBAZI MATANO YAUAWA NA POLISI JIJINI MBEYA JANA MCHANA

Kamanda diwani akiwaonyesha moja ya jambazi lililokuwa limeshika silaha



Hii ndiyo Gari iliyotumiwa na majambazi hayo
Siraha walizokuwa wanatumia majambazi hayo

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amewaambia Wandishi wa Habari Ofisini kwake kuwa Tukio hilo limetokea leo majira ya saa Sita Mchana katika kijiji cha Garijembe Wilaya ya Mbeya katika Barabara ya Mbeya Tukuyu.




MTANDAO wa Ujambazi nchini hususani Mkoani Mbeya umezidi kusambaratishwa  baada ya watu watano wanaodhahaniwa kuwa ni majambazi kuuawa katika majibizano na Askari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya.
 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amewaambia Wandishi wa Habari Ofisini kwake kuwa Tukio hilo limetokea leo majira ya saa Sita Mchana katika kijiji cha Garijembe Wilaya ya Mbeya katika Barabara ya Mbeya Tukuyu.

 
Alisema baada  ya  Jeshi la Polisi kupata taarifa za Kinterejensia waliweka mitego mbali mbali na kufanikiwa kuwanasa watu hao wakiwa kwenye gari lenye  namba za usajili T  911 BUG aina ya Toyota Spacio.....


Baada ya kusimamishwa ghafla walianza kurusha risasi ovyo  ambapo Askari walijibu mapigo na kufanikiwa kuwajeruhi wote watano ambapo waliwafikisha katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa ajili ya Matibabu lakini Daktari alithibitisha kuwa tayari walikuwa wamekufa.
Aliongeza kuwa baada ya kufanyiwa upekuzi walikutwa na Silaha mbili ambazo ni bunduki aina ya SMG 848628 ambapo kwenye magazine zilibaki risasi 16 na bunduki nyingine aina ya Mark III yenye namba 94695J ikiwa na risasi mbili pamoja na Koa za Shaba.
 
Kamanda Diwani ameongeza kuwa taarifa za Kinterejensia zilieleza kuwa majambazi hayo yalijipanga kufanya uhalifu katika maeneo ya Ushirika, Tukuyu Mjini Wilayani Rungwe pamoja na Eneo la Uyole Jijini Mbeya.
 
Aidha alisema majina yao wala makazi yao hayakuweza kujulikana mara moja ambapo miili  yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na kutoa wito kwa wananchi kufika Hospitalini hapo kwa ajili ya kuwatambua ndugu zao ili wakabidhiwe kwa taratibu za mazishi.
 
Pia anatoa wito kwa wananchi wenye taarifa zinazohusu uhalifu kuzitoa katika mamlaka zinazohusika kwa wakati ili zifanyiwe kazi.

MFANYABIASHARA KARIAKOO AJIRUSHA TOKA GHOROFA YA TISA NA KUANGUKIA GARI MCHANA HUU

Muda mfupi uliopita,Mtu mmoja alietambulika kwa jina la Shirima ambaye ni Mfanyabiashara katika moja ya Maduka ya Kariakoo jijini Dar es Salaam,amejirusha toka ghorofa ya 9 ya Hoteli ya Concord iliopo Maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam na amekimbizwa hospitali kwa uangalizi zaidi maana haijafahamika kama kapoteza Maisha au bado yu hai.

Mfanyabiashara huyo alijirusha toka ghorofani na kuangukia Gari aina ya Toyota Corolla ambayo ni taxi iliyokuwa imepaki nje ya hoteli hiyo....chanzo cha kujirusha kwa mfanyabiashara huyo bado hakijafahamika mpaka sasa.

Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea muda mfupi uliopita,wanaeleza kuwa walipatwa na mshuko baada ya kusikika kishindo cha kitu kilichokuwa kimeangukia gari hilo na waliposogea kushuhudia ndipo walipobaini kuwa alikuwa ni mtu huyo alietambulika kwa jina moja la Shirima.

Wednesday, May 1, 2013

AIBU: MWANAUME AFUMANIWA NA MKE WA MTU GESTI AKIWA UCHI WA MNYAMA



Habari kamili zilizonaswa  na  waandishi  wetu  ni kwamba mwanaume aliyetajwa kwa jina la Baba Asha alidai kumfumania rafiki yake wa karibu, Baba Tony akiwa gesti na mkewe (jina linahifadhiwa), tayari kwa kuvunja naye amri ya sita. 
 
Tukio hilo la aibu ya milenia lilijiri katika nyumba ya kulala wageni ya Pumzika iliyopo maeneo ya Msimbazi Center, jijini Dar ambapo mara baada ya kumtia mikononi ‘mwizi’ wake ambaye mbali na urafiki pia ni majirani, ndipo akamchakaza sura vibaya na kumsababishia kuvuja damu.
 
Habari za kina zilidai kuwa mke wa Baba Asha alikuwa bafuni akioga, mara ukaingia ujumbe mfupi ‘sms’ kwenye simu yake ya kiganjani, ndipo mumewe akachukua kilongalonga hicho na kuufungua ujumbe huo.
 
Ilidaiwa kuwa mume alitaharuki kukutana na ujumbe uliokuwa ukimtaka mkewe kwenda Pumzika Guest House kukutana na jamaa huyo.
 
Iliendelea kudaiwa kuwa Baba Asha hakuyaamini macho yake, akausoma tena ule ujumbe na ndipo akagundua sms nyingine nyingi, vocha na fedha za mtandao alizokuwa akitumiwa mke wake kutoka kwa Baba Tony.
 
Chanzo kilidadavua kuwa baada ya kugundua mchezo mzima, Baba Asha akatulia na kumsubiri mkewe atoke bafuni ili kuliweka sawa suala hilo.
Ilifahamika kuwa mke aliporudi kutoka kuoga, mume hakuonesha dalili zozote, alichokifanya ni kumwita mkewe na kumwambia kuwa achague moja, kufungasha kilicho chake, aondoke nyumbani kwake au amwekee jamaa mtego anaswe ili ajue mke wa mtu ni sumu.
Jibu lilikuwa rahisi kwani alikubali kuweka mtego ili amnase mbaya wake ndipo atamsamehe.

Ilifahamika kuwa ilipita wiki moja kimyakimya kwani mara ya kwanza Baba Tony alichezwa na machale, alipofika kwenye gesti hiyo na kumwona mtu anayemfahamu, alimwambia yule mwanamke waahirishe.

Habari za uhakika ni kwamba wiki iliyopita, Baba Tony aliingia kwenye kumi nane, akajaa mzimamzima kwenye mtego wa fumanizi uliowekwa na Baba Asha na mkewe.

Mara baada ya kuona mwanaume mmoja (Baba Asha) akiwa na askari kwenye gesti hiyo akihaha, king’ora kililia kwenye akili ya mwandishi wetu ambaye hakufanya makosa, akamfuata mfumaniaji kwa nyuma hadi aliporuhusiwa kumfuata mkewe chumbani.

Chumbani mtiti ulikuwa mkubwa ambapo Baba Tony alikutwa kama alivyozaliwa huku mke wa mtu akiwa bado hajavua na ndipo mtiti ukaanza.
 Katika purukushani, Baba Asha alimpa kibano ‘mwizi’ wake hadi akamchana usoni na kumng’oa meno ya mbele, jambo lililosababisha kutokwa na damu nyingi.

Kama hiyo haitoshi, ili kuthibitisha kuwa mke wa mtu ni sumu, Baba Asha alimchoma jamaa huyo bisibisi kwenye makalio hadi askari alipoingilia kati na kumchukua mtuhumiwa kisha akamtoa nje.
Wakiwa nje ya gesti hiyo, Baba Tony aliomba kujisafisha damu na baada ya hapo alipigwa pingu tayari kwa kupelekwa Kituo cha Polisi, Pangani, Ilala...

HUU NDO WARAKA WA LADY JAYDEE:::WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA,USOME HAPA.

Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.


Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.


Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.

Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.


Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria.

Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu.


Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia.

Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa,
Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa.

Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao.

Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni.


Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu.


Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige wame

Enyi mtakaokuwa hai baada yangu.


Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai

Hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu.

Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia.


Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge.

Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka.


Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha,
Hamuwezi kumiliki dunia..
Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star..


Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie??.

Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu.


Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili.

Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri.

Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani??

Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi??


Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili.


Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu.

Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma??

Roho gani hiyo??


Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu


JIDE

LEMA KUMBURUZA MKUU WA MKOA WA ARUSHA MAHAKAMANI.

Akizungumza na waandishi wa habari hii jana katika ofisi ya CHADEMA mkoa mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema ameelezea nia yake ya kumshitaki, Magesa Mulongo kwa kumtumia ujumbe wa matisho katika simu yake ya mkononi.   
 
Ameeleza kuwa Mulongo ametumia kila njia kutafuta simu yake ikiwa ni pamoja na kutaka kumrubuni mke wake na pia kumtumia Mbunge wa Arumeru Mashariki kuzungumza nao ili simu iyo iwasilishwe polisi ila imeshindikana.

'Wanasheria wangu wapo katika hatua za mwisho kuandaa mashitaka dhidi ya Mulongo' amedai kamanda Lema..miongoni mwa mawakili wa Lema atakuwepo Kamanda Tundu Lissu