Wednesday, April 24, 2013

PICHA: HUU NDO UNYAMA WALIOTENDEWA WANAFUNZI WA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

Picha  ya  marehemu  Henry Koga  baada  ya  kuchomwa  kisu  na  kufariki  hapo hapo  jana  usiku  katika  chuo  cha  uhasibu  Arusha.....


Mwanafunzi  huyo  Alikuwa Masomoni Mida Ya Usiku Na Alipomaliza Aliondoka Na Kuelekea Maeneo Ya Esami. Kabla Hajafika Eneo La Malazi (Hostel) alipigiwa Simu na Mwenzake amsubiri Ili Waende Wote Hostel. 

Wakati anamsubiri Rafiki Yake Kwenda Hostel, Kuna Bajaj Ilifika Eneo Hilo Na Watu Hao Wasiojulikana Wakataka Pesa Kutoka Kwa Mwanafunzi Huyo...Wakati  wakiendelea  kuzozana, rafiki  yake  naye  alifika.....
 
Majibu Ya Wanafunzi HaoHayakuwafurahisha Watu Hao Na Ndio Walipochomoa Kisu Na Kumchoma Mmoja wa Vijana Hao Tumboni Na Shingoni na Kupoteza Maisha Hapo Hapo....

Mauaji  hayo  yamesababisha  vurugu  kubwa  chuoni  hapo  zilizopelekea  kupigwa  mawe  mkuu wa  mkoa 


   Marehemu  Henry  katika enzi za uhai wake....

MAUAJI YA KUTISHA CHUO CHA UHASIBU




Huyu Ndio Henry Aliye Uawa


Mbunge Wa Arusha Mjini Godbless Lema Akiwatuliza Wanafunzi Wa Chuo Hicho

----

Taarifa Kutoka  Chuo Cha Uhasibu Arusha zinadai kuwa Mwanafunzi Wa BEF 2  anayejulikana  kwa  jina  la  Henry  ameuawa  kikatili  na  watu  wasiofahamika....

Mwanafunzi  huyo  Alikuwa Masomoni Mida Ya Usiku Na Alipomaliza Aliondoka Na Kuelekea Maeneo Ya Esami. Kabla Hajafika Eneo La Malazi (Hostel) alipigiwa Simu na Mwenzake amsubiri Ili Waende Wote Hostel.  
 
 Inasemekana Wakati anamsubiri Rafiki Yake Kwenda Hostel, Kuna Bajaj Ilifika Eneo Hilo Na Watu Hao Wasiojulikana Wakataka Pesa Kutoka Kwa Mwanafunzi Huyo...Wakati  wakiendelea  kuzozana, rafiki  yake  naye  alifika.....
 
Majibu Ya Wanafunzi Hao Hayakuwafurahisha Watu Hao Na Ndio Walipochomoa Kisu Na Kumchoma Mmoja wa Vijana Hao Tumboni Na Shingoni na Kupoteza Maisha Hapo Hapo....

 
Rafiki Aliye Kuwa Nae Inasemekana Alichomwa Kisu Cha Tumboni Na Kuachwa Akishuhudia Mwenzake Akipoteza Maisha.

VURUGU KUBWA CHUO CHA UHASIBU:....MKUU WA MKOA APIGWA MAWE, GODBLESS LEMA AFICHWA..!!


Vurugu  kubwa  zimeibuka  chuo  cha  uhasibu cha Arusha   baada ya mwanachuo kuchomwa kisu na mwanaakijiji na kufariki dunia....

Baada  ya  tukio  hilo, wanafunzi  walitoa  taarifa  kwa  mkuu wa chuo lakini  hakuwapa msaada wowote.


Walipokosa  msaada,wanafunzi  hao walianza  kuandamana  na taarifa zikafikishwa kwa mbunge  Godbless  lema ....


Mbunge  huyo  bila   hiyana akawasili na kufanikiwa kuwatuliza wanachuo hao maana nyumbani kwa Godbless  lema si mbali na chuo hicho ...

Baada  ya  taarifa  kumfikia Mkuu wa mkoa, ilimbidi  aliwasili na kuanza kuzungumza na wanachuo lakini baada ya kugundua uwepo wa Lema alianza kuongea  kwa  lugha  mbovu  na  ndipo wanachuo walipo kasirika na kuanza kumpiga mawe.


Hali  ilipochafuka,FFU  waliingia kazi  ya  kutuliza  ghasia...Hali ni mbaya sana lakini cha kushangaza askari mmoja aliwatonya wanachuo wamfiche Lema


Godbless  Lema  anasakwa mpaka sasana  hajulikani alipo baada ya wanachuo kumficha kusiko julikana.